
Kizazi njia panda - Awamu ya 1: Maamuzi magumu yanayotukabili
Bongo Academy ni shule ya fahari. Ni shuleni hapo wanapokutana nyota wa mchezo huu Mercy, Trudy, Dan na Niki - vijana wanne wanaotoka kwenye mazingira na matabaka tofauti. Na wala hawajui changamoto zinazowasubiri.
“Nimesimama kwenye njia panda, nikijaribu kuwa jasiri. Nigeukie wapi? Natokea wapi?'' Mashairi haya ya muziki wa Rap katika mchezo wa kuigiza wa “Kizazi Njia Panda”, yanaonyesha ukweli wa mambo. Yametolewa na mmoja wa vijana waigizaji kwenye mfululizo wa vipindi vipya vya Noa Bongo Jenga Maisha Yako, kueleza hali ngumu wanayokutana nayo vijana wa Afrika kila siku wanapochukua maamuzi kuhusu mkondo upi wa maisha wanapaswa kuufuata.
“Nimesimama kwenye njia panda, nikijaribu kuwa jasiri. Nigeukie wapi? Natokea wapi?'' Mashairi haya ya muziki wa Rap katika mchezo wa kuigiza wa “Kizazi Njia Panda”, yanaonyesha ukweli wa mambo. Yametolewa na mmoja wa vijana waigizaji kwenye mfululizo wa vipindi vipya vya Noa Bongo Jenga Maisha Yako, kueleza hali ngumu wanayokutana nayo vijana wa Afrika kila siku wanapochukua maamuzi kuhusu mkondo upi wa maisha wanapaswa kuufuata.